Psalms 126:1-3

Kurejezwa Kutoka Utumwani

Wimbo wa kwenda juu.

1 a Bwana alipowarejeza mateka Sayuni,
tulikuwa kama watu walioota ndoto.
2 bVinywa vyetu vilijaa kicheko,
ndimi zetu zilijaa nyimbo za shangwe.
Ndipo iliposemwa miongoni mwa mataifa,
Bwana amewatendea mambo makuu.”
3 c Bwana ametutendea mambo makuu,
nasi tumejaa furaha.
Copyright information for SwhNEN